Heade

FAIDA YA KUFUATA RATIBA YA CHAKULA KWA AFYA BORA



FAIDA ZA KUFUATA RATIBA YA CHAKULA KWA AFYA BORA.
Ili kuwa na afya njema ni muhimu kula vizuri . kula vizuri si rahisi ingawa wengi wetu tunadhani kula vizuri ni kula chips, kuku, au mayai na vingine haya ni mazoea mabovu.
kula vizuri si lazima kula vyakula unavyovipenda bali ni kula vyakula vyenye afya na kujenga mwili wako. njia moja mbadala ya kuhakikisha unakula vizuri na kwa afya ni kuwa na ratiba ya wiki ya chakula.
FAIDA ZA KUFUATA RATIBA YA CHAKULA.
Kufahamu kirahisi ni vyakula vipi vyenye afya na mahitaji yako mfano mzuri ni kuwa na uwezo wa kula matunda na vyakula vya protini kwa wingi.
Ni rahisi kujua virubisho muhimu unavyokula kwa kipindi cha wiki nzima hivyo ni rahisi kukusaidia kutathmini afya yako kwa uraisi.
Kuwa na chaguo zaidi ya moja ya vyakula hivyo na kuzuia kula chakula cha aina moja kinachopendelewa na kusababisha kukosa virutubisho muhimu kwenye vyakula vingine.
Kudumisha furaha nyumbani kwa sababu kila mmoja ataona umuhimu wake katika mawazo juu ya chakula, hivyo kuwafanya watu kufurahia kujumuika kula pamoja kifamilia.
NB;
Ni vizuri kuwa na ratiba ya chakula kwa wiki nzima hii itasaidia kujua milo ya chakula kila siku na jumla ya virurubisho unavyopata mwilini .
Ratiba ya wiki itakusaidia kujua ni kiasi gani cha chakula kinahitajika mwilini mwako kama uko peke yako au na familia.
JINSI YA KUANDAA RATIBA YA CHAKULA.
Hakikisha unapata vyakula muhimu. Angalia aina za vyakula kwa siku matunda na mboga mboga hizi ni muhimu kuwepo kwa sababu zina virutubisho halisi vinavyohitajika mwilini.
Pendelea vyakula halisi (Natural foods). Ni rahisi sana kula vyakula visivyo na virutubisho nyumbani sababu ndivyo vyakula vilivyojaa kila kona ya dunia kwa sasa.Ili kuwa na afya bora pendelea zaidi kula vyakula halisi kuliko vile vya kuchakachua, kunywa maji ni muhimu sana lakini wengi tunapuuzia hii kanuni ya afya mfano mtu mzima anatakiwa kunywa maji lita moja na nusu kwa siku ingawa wengi wanapendelea kunywa maji pale wanapohisi kiu tu.
Kuwa mbunifu.
kula ni haki yako lakini kwanini ule chakula cha aina moja wakati kuna vyakula vingi vya kuijenga afya yako? cha muhimu ni kujifunza kuandaa vyakula tofautitofauti ,kula vyakula aina mbalimbali ili kuweza kutimiza hili, jaribu kula vyakula tofauti kutokana na ratiba yako na ni muhimu kutopendelea vyakula kwenye kundi moja sababu unakosa virutubisho kutoka kwenye makundi mengine.
NB;
UNASHURIWA UWE NA RATIBA YA CHAKULA NYUMBANI NA NI VIZURI KWA AFYA PIA KWA  KUJUA MATUMIZI YA NYUMBANI , ME HUWA NAFANYA HIVI KILA WAKATI NA NIMEONA FAIDA ZAKE NA NDIO MAANA NAKUSHAURI NA WEWE KAMA UNAPENDA BASI WASHAURI NA WENZIO KWANI KILA KIZURI NI VIZURI KUWAELEZA NA WENZIO. BY levyzevoice@.com ,mobile phone:0759820684

No comments

Powered by Blogger.