Heade

BENKI NA TAASISI ZA FEDHA ZATAKIWA KUTOA MIKOPO KWA WAFANYABIASHARA WA CHINI NA WA KATI.



WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amezitaka benki na taasisi za fedha nchini kuanza kuweka mikakati ya makusudi ya kushirikiana na serikali katika kuiwezesha Tanzania kuwa nchi ya viwanda

Akizungumza katika maadhimisho ya miaka 10 ya kuanzishwa kwa benki ya Afrika BOA tawi la Tanzania  jijini Dar es salaam  amesema ni vema taasisi za fedha na mabenki yakaanza kutoa mikopo kwa wafanyabiashara wa chini na wa kati ili kuwawezesha kuanzisha viwanda vya kati hiyo badala ya kushughulika na wafanyabiashara wakubwa ambao ni wachache.

Aidha  waziri Mwijage amesema serikali ina mkakati wa kuangalia upya mazingira ya ufanyaji biashara nchini ili kuboresha zaidi mazingira hayo kwa lengo la kuondoa urasimu na kuvutia uwekezaji zaidi nchini huku akiipongeza Benki ya Afrika kwa kutoa huduma nzuri kwa watanzania suala ambalo limechochea kuinua hali ya maisha ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Naye  mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Ammish Owusu Amoah amesema benki hiyo imefanikiwa kuwa benki ya kipekee na mfano katika uwepo wake nchini kutokana na kutoa huduma za kipekee na kwa asilimia 100 ukilinganisha na benki nyingine ambazo zinafikia asilimia kati ya 70 na 80 ya utoaji wa huduma.

No comments

Powered by Blogger.