Heade

WAKIMBIZI 57000 WAKIMBILIA UGANDA


Zaidi ya wakimbizi Elfu hamsini na saba wamekimbilia nchini Uganda mwaka huu baada ya kushuhudia machafuko ya kikabila katika jimbo la Ituri kaskazini mashariki mwa Jamuhuri ya Demokrasia ya Congo,kulingana na shirika la Umoja wa mataifa linalohudumia wakimbizi UNHCR.

Idadi ya wakimbizi wa mwaka huu inapita wakimbizi 44,000 ambao walifanya safari kama hiyo katika kipindi cha mwaka 2017 kwa mujibu wa msemaji wa UNHCR Babar Baloch, Wakimbizi wamekuwa wakiingia nchini Uganda kupitia ziwa Albert na kuhatarisha maisha yao mara kadhaa.

Mapigano jimboni Ituri yamehusisha jamii ya Hema na Lendu ambao ni wakulima na wafugaji wenye historia ndefu tangu kuanza kwa uhasama wakigombania ardhi kaskazini mashariki mwa Jamuhuri ya Demokrasia ya Congo.

No comments

Powered by Blogger.