Heade

TANESCO WATAKIWA KUWAFUATA WANANCHI VIJIJINI.



WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) liwafuate wananchi walioko katika vijiji vinavyotarajiwa kuunganishiwa umeme kupitia Wakala wa Nishati Vijijini REA.

Amesema serikali imetenga shilingi trilioni moja kwa ajili ya kusambaza umeme katika vijiji vyote ambavyo havijaunganishiwa nishati hiyo nchini, hivyo ni vema wakawatembelea wananchi katika maeneo yao na kuwahudumia.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo  kwenye mkutano wa hadhara  katika uwanja wa michezo Tunduru  huku akiwasisitiza watumishi wa TANESCO kutokaa maofisini na badala yake wakawahudumie wananchi katika maeneo yao.
Amesema serikali imedhamiria kusambaza huduma ya nishati ya umeme katika vijiji vyote nchini, vikiwemo vya wilaya ya Tunduru ambapo wananchi hao wataunganishiwa umeme huo kwa gharama ya Sh 27,000 tu.

No comments

Powered by Blogger.