Heade

MARUFUKU KUAGIZA TRANSFOMA NGUZO NA VIFAA VINGINE VYA UMEME KUTOKA NJE YA NCHI



Waziri wa nishati Dk Medard Kalemani amepiga marufuku kwa shirika la umeme TANESCO na wakala wa umeme vijijini REA kuacha kuagiza transfoma ,nguzo na vifaa vingine kutoka nje ya nchi ili kudhibiti uingizwaji holela wa vifaa visivyo na ubora vinavyoathiri na kudidimiza uchumi wa ndani.
Ametoa rai hiyo baada ya kutembelea kiwanda cha kutengenezea transfoma TANALEC kilichopo jijini Arusha amesema serikali imepata hasara kubwa kwa uingizwaji wa transfoma kutoka nje ambapo hivi karibuni zaidi ya transfoma 20 ziliingizwa hapa nchini na kugundulika kuwa ziko chini ya kiwango.
Mkurugenzi wa TANALEC Zahri Salehe amesema wanajipanga kuzalisha Transfoma za kutosha ili kumudu soko la ndani huku naye mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema serikali ya mkoa huo itahakikisha inasimamia utekelezaji wa agizo hilo.

No comments

Powered by Blogger.