Heade

MIMBA ZA UTOTONI BADO NI TISHIO MKOANI KATAVI



Mkuu wa mkoa wa katavi Meja Jenerali Msataafu Raphael Muhaga amesema kuwa mimba za utotoni bado ni tishio kubwa katika manispaa ya mpanda mkoani Katavi ambako wasichana 624 walio na umri chini ya miaka 18 wamejifungua katika vituo vya afya vilivyopo katika manispaa hiyo.
Hayo ameyasema wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia mkoani humo katika viwanja vya sabasaba kabungu wilayani tanganyika.
Meja jenerali Muhaga amesema kuwa taarifa kutoka katika vituo vya afya vya manispaa ya mpanda ya kipindi cha mwaka jana inaonyesha wasichana 624 walijifungua kiwango ambacho ni  tishio katika mkoa wa katavi.
Aidha kuhusu unyanyasi wa kijinsia amesema kuwa kesi 1,178 zimeripotiwa katika vituo vya kutolea huduma za afya mkoani humo na maofisa ustawi wa jamii mwaka 2016.
Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoa wa katavi Damas Nyanda amesema licha ya jitihada zinazochukuliwa na serikali kwa kushirikiana na makundi mbalimbali ya kijamii takwimu bado zinaonyesha ongezeko la ukatili wa kijinsia kuwa kubwa.

No comments

Powered by Blogger.