Heade

MASHIRIKA YANAYOTETEA HAKI ZA BINADAMU YAMETAKIWA KUTOUWEKA MBALI UKATILI WA KIUCHUMI



Mkuu wa mkoa wa kilimanjaro Anna mghwira ameyataka mashirika yanayotetea haki za binadamu na yanayopinga vitendo vya ukatili wa kijinsia katika mikoa ya kanda ya kaskazini kutouweka pembeni ukatili wa kiuchumi kwani ndio unaozaa ukatili mwingine.
 Ameyazungumza hayo akiwa katika stendi kuu ya mabasi  moshi mjini, yaendayo mikoani wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Ameongeza kuwa katika uongozi wa awamu ya tano mhe, rais Magufuli amekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha anapambana kumaliza ukatili wa kiuchumi katika migodi ya madini na dhahabu kwani rasilimali za nchi zilikuwa hazimnufaishi mwananchi.
Amewataka watu wa mashirika ya kutetea haki za binadamu kuzungumzia suala la ukatili wa kiuchumi.

Maaadhimisho hayo yanaratibiwa na shirika la kilimanjaro women information exchange and comunity organisation yakihusisha mikoa ya kilimanjaro,Arusha, Tanga,na Manyara ambayo hufanyika kila mwaka.

No comments

Powered by Blogger.