Heade

MNANGAGWA ATARAJIWA KUAPISHWA KUWA RAIS WA ZIMBABWE



Aliyekuwa makamu wa rais nchini Zimbabwe Emmerson Mnangagwa ambaye kufutwa kazi kwake kulichochea mgogoro wa kisiasa nchini Zimbabwe na kupelekea jeshi kuchukua udhibiti wa madaraka  anatarajiwa kuapishwa kuwa rais wa nchi hiyo.
Hatua hiyo inafikiwa baada ya Robart Mugabe  aliyeiongoza nchi hiyo kwa muda mrefu kujiuzulu baada ya kuwepo kwa  maandamano ya wananchi wa Taifa hilo wakishinikiza aachie ngazi hali iliyochochewa na kile kinachodaiwa kuwa alitaka kumrithisha kiti hicho mke wake bi Grace Mugabe.
Mnangagwa amesema kipaombele chake ni kujenga upya uchumi wa nchi hiyo na kuunda ajira mpya kwa idadi kubwa ya watu wasio na ajira na kulishukuru jeshi la nchi hiyo kuliingilia kati baada ya baada ya yeye kufukuzwa na rais Robart Mugabe.

No comments

Powered by Blogger.