Viongozi wa Mashtaka nchini Afrika Kusini wamesema
wametoa muda zaidi kwa rais Jacob Zuma, kuwasilisha utetezi wake kuhusu
kufunguliwa kwake mashitaka ya ufisadi.
Zuma amepewa hadi tarehe 31 mwezi Januari mwaka 2018, kuwaridhisha viongozi wa mashtaka wasimfungulie mashtaka hayo.
Rais
Zuma, anadaiwa kuhusika katika visa 783 za ufisadi zenye thamani ya
Dola za Marekani Bilioni 2.20 katika mkataba wa kununua silaha alipokuwa
Waziri miaka 1990.
Viongozi wa mashtaka walilazimika, kusitisha mpango wa kumfungulia Zuma kesi alipokuwa anajiandaa kuwania uraia mwaka 2009.
Hata hivyo, rais Zuma ameendelea kukanusha madai ya ufisadi dhidi yake.
Rais Zuma, anaandamwa wakati huu anapokaribia kuondoka madarakani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2019.
Wiki
hii, rais Zuma atamaliza muda wake katika mwenyekiti wa chama tawala
ANC, nafasi ambayo huenda ikachukuliwa na naibu wake Cyril Ramaphosa
ambaye pia amekuwa akimshutumu Zuma kwa kuhusika na ufisadi.
No comments