Heade

WANAWAKE WATATU WAMTUHUMU RAIS TRUMP

Wanawake watatu wamejitokeza na kumtuhumu rais Donald Trump kwamba aliwafanyia ukatili wa kijinisa bila ridhaa yao miaka iliyopita,

 huku wakiombabunge la wawakilishi kumchunguza kutokana na kashfa hizo.

Jessica Leeds, Samantha Holvey, na Rachel Crooks wamesema kuwa rais Trump alikuwa akiwabusu kwa nguvu akiwashika shika na kuwafanyia ukatili mwingine.

Hata hivyo msemaji wa ikulu ya White House, Sarah Huckabee Sanders, amesema kuwa madai hayo hayana msingi wowote na ni uzushi.

Baadhi ya wanawake hao wamedai kuwa walilazimishwa kufanyiwa ukatili huo kama vile kupigwa busu na ukatili mwingine.

Samantha Holvey amesema, Trump alikuwa akiwakagua mwilini wakati alipokua akihudhuria mashindano ya Wasichana Warembo mwaka 2006. Lakini amesema hana nia ya “kumchukulia hatua bali anaweka wazi dhulma aliofanyiwa.

Rais Trump tangu achukue hatamu ya uongozi wa Marekani amekua akikabiliwa na tuhuma kama hizi ikiwa ni pamoja na kashfa za ukwepaji kodi na zile za kisiasa.

No comments

Powered by Blogger.