Hatua ya Marekani ya kuhamisha ubalozi wake katika
mji wa Jerusalemu na kutambua mji huo kama mji mkuu wa Israel
itasababisha janga kwa eneo hilo, amesema jana jumanne Rais wa Iran,
Hassan Rohani.
"Tunapaswa
kusimama dhidi ya uamuzi huu mbaya, tukiushtumu kwa sauti moja, tukisema
kwamba hilo haliwezekani," Hassan Rohani amesema katika taarifa
uliyorushwa kwenye runinga ya taifa., nchini Uturuki, ambapo atashiriki
katika mkutano wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC) kesho Jumatano,
mkutano ambao utajadili kuhusu uamuzi wa Marekani juu ya Jerusalem.
Waziri
wa Ulinzi wa Iran, Amir Hatami, alisema siku ya Jumatatu kuwa uamuzi wa
rais wa Marekani Donald Trump kutambua Jerusalem kama mji mkuu wa
Israeli utasababisha kufutwa au kuangamizwa kwa taifa la Israel. Kwa
upande wake, afisa mwandamizi wa Kikosi cha jeshi la Ulinzi wa Mapinduzi
cha Iran aliwapiga simu viongozi wa makundi mawili yenye silaha ya
Palestina kuwajulisha kuhusu kuungwa mkono na nchi yake.
"Kutokana na uamuzi huu usiofaa, mbaya na usio halali, Waislamu walikaa kimya (...)," alisema.
"Ni mtihani kwa Waislamu na ulimwengu wa Kiislam kwa ujumla, pamoja na Wapalestina," aliuongeza.
No comments