Heade

TATIZO LA AJIRA NCHINI LAPUNGUA


Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema tatizo la ukosefu wa ajiri nchini limepungua.

Mkurugenzi wa Shughuli za Takwimu, NBS Irineus Ruyoby amesema kwa mujibu wa takwimu walizonazo kwa sasa zinaonyesha tatizo la ukosefu ajira linaenda likipungua mwaka hadi mwaka.

“Takwimu ambazo tunazo zinaonyesha kiwango cha watu ambao hawaja ajiriwa kimepungua mwaka hadi mwaka, sasa hivi tupo katika kufanya tafiti nyingine tutaweza kujua hali halisi sasa ikoje” amesema.

Ameongeza kuwa uchumi wa Tanzania kwa sasa unaendelea kukua kwa kiwango cha wastani wa asilimia saba kwa mwaka na imekuwa hivyo kwa muda mrefu sasa.

No comments

Powered by Blogger.