Heade

YANAYOKUPATA YANATOKA UNAPOKAA



        YANAYOKUPATA YANATOKA UNAPO KAA
Kuna mambo mengi yanayoweza kumpata mtu, mambo haya yanaweza kuwa mazuri yanayomfaa na kumpendeza au mabaya yasiyostahili kumkuta mwanadamu awaye yote hapa duniani.
Mambo menge yanayompata mtu yanatoka mahali anapokaa au anapopendelea kuwa mara nyingi.
Kuna watu wamepatwa na misukosuko na wengine kupoteza  baadhi ya viungo vya sehemu za miili yao hata maisha, kutokana na ugomvi uliotokea katika vijiwe wanavyo kaa , wengine wamekutwa na hatia wameangukia kifungo kwa matukio mabaya yaliyo tokea, mahali au kijiweni wanakokaa.
Vijana wengi wamepoteza mwelekeo wa maisha na hata kuzisababishia familia zao matatizo makubwa kwa kupotoshwa na makundi wanayoyapendelea kukaa.
Wengine wameingia katika ugomvi mbaya katika familia na ndoa zao zimeharibika na kusambaratika kabisa kutokana na kupata ushauri mbaya kutoka walikopendelea kukaa mara nyingi.
Wengi wamejikuta wakifilisika na kuishi maisha ya umasikini chanzo kikiwa ni mahali walipopendelea kukaa wakati wakiwa na mali.
Hata magonjwa mabaya na ya kutisha yamewapata wengi chanzo ni mahali walipopendelea kukaa.
Ukisoma Biblia takatifu Marko 5:1-5, utaona habari za mtu aliyekaa makaburini, makaburini ni sehemu inakowekwa miili ya watu waliofariki, si eneo la kukaa watu lakini mtu huyu alikaa makaburini, neno linasema;-Na siku zote, usiku na mchana alikuwako makaburini na milimani akipiga kelele na kujikata kata kwa mawe.
Marko5:4 inasema;-mtu huyu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, akaikata ile minyororo na kuzivunja vunja zile pingu wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu ya kumshinda.
Usishangae kumwona kijana anashauriwa na wazazi wake lakini hasikii lolote na wala hajali,ndungu wamemshauri mwana familia wamekaa vikao visivyoweza kuhesabika lakini hana wakumsikia, anaendelea kufanya jinsi apendavyo mwenyewe, ni kwambie kwamba, mahali anapopendelea kukaa pamemfanya awe jinsi alivyo. 
Mahali unapokaa panaweza kukufanya ufanye vitu vibaya vinavyo yaghalimu maisha yako ni vyema na muhimu sana kutathimini kwa kina faida unayoipata kutokana na sehemu au mahali unapopendelea kukaa mara kwa mara.
 Na ukweli ni kwamba watu wengi wako jinsi walivyo kutokana na mahali wanapopendelea kukaa na hata wewe huenda uko hivyo ulivyo kutokana na hapo unapopapendele kukaa hivyo fanya uchunguzi kubaini kama unavuna mabaya au mema kutoka sehemu au mahali unapopendelea kukaa muda mwingi.
jamesmtiba@ gmail .com

No comments

Powered by Blogger.