MELI YA MAFUTA ILIYOKUA INATEKETEA KWA MOTO IMEZAMA BAHARINI
Meli ya mafuta ambayo imekuwa ikiteketea kusini mwa bahari ya China kwa zaidi ya wiki moja hatimaye imezana, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya China.
Sanchi na meli nyingine ya mizigo ziligongana kilomita 260 nje ya Shanghai tarehe 6 Januari ambapo baadaye ilianza kusombwa kusini mashariki kwenda Japan.
- Meli ya kubeba mafuta bado yateketea moto pwani mwa China
- Meli ya mafuta na ya mizigo zagongana China
Maafisa wa Iran sasa wanasema kuwa wahudumu wote 32, wakiwemo raia 30 wa Iran na wawili raia wa Bangladesh wote walifariki.
Meli hiyo ilikuwa imebeba tani 136,000 za mafuta lakini maafisa wanasema kuwa hakuna hatari kubwa.
No comments