Heade

RAILA ODINGA AMEKUTANA NA MWENYEKITI WA TUME YA UCHAGUZI (IEBC) NCHINI KENYA

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini kenya Wafula Chebukati amekutana na mgombea urais wa upinzani Raila Odinga  na kusema anatarajia kukutana na mgombea wa chama Tawala cha Jubilee Uhuru Kenyata.
Mwenyekiti huyo ameitisha mkutano wa wagombea urais wote leo mchana lakini akauhairisha mapema.
Hatahivyo rais Kenyata amesisitiza yuko tayari kwa uchaguzi huo na utaendelea pamoja na kuwa  mgombea wa upinzani Raila Odinga alijiondoa wiki iliyopita.
Upande wa upinzani umekuwa ukishinikiza kuondolewa kwa afsa mkuu mtendaji wa tume hiyo Ezra Chiloba na maafsa wengine hatua ambayo haijatekelezwa na ndiyo sababu kubwa iliyomfanya kinara wa upinzani Raila Odinga asusie kushiriki katika uchaguzi wa marudio uliopangwa kufanyika  Oktoba 26 mwaka huu.

Hata hivyo hali hiyo imezidi kuumiza vichwa kwa pande zote mbili na kuyafanya Mataifa mengi ndani na nje ya Afrika kuitupia nchi hiyo macho kila uchao huku Uhuru Kenyata akiwaomba  viongozi wa dini nchini humo  kuwaongoza waumini wao kuliombea Taifa hilo.

No comments

Powered by Blogger.