Heade

MUGABE AONEKANA HADHARANI



Rais wa Zimbabwe Robart Mugabe leo ameonekana kwa mara ya kwanza tangu jeshi la nchi hiyo lichukue udhibiti wa nchi ikiwemo kituo cha Runinga cha Taifa nchini humo toka siku ya jumatano.
Bwana Mugabe amekua chini ya kizuizi cha nyumbani kwa siku kadhaa huku kukiwa na mvutano wa  nani atakae mrithi.
Jeshi la Zimbabwe limesema lilikua kwenye mazungumzo na Mugabe na litaujulisha umma matokeo ya mazungumzo hayo.
Rais huyo aliyedumu madarakani kwa muda mrefu na mwenye umri mkubwa Duniani alianza kuiongoza Zimbabwe tangu mwaka 1980.

No comments

Powered by Blogger.