Heade

SERIKALI IMEWEKA MIKAKATI ENDELEVU KUPUNGUZA VIFO VYA WATOTO NJITI



.
Mkurugenzi wa huduma za kinga katika wizara ya afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Dkt. Neema Rusibamayala. Amesema serikali imeweka mikakati endelevu ya kupunguza vifo vya watoto njiti kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya afya nchini.
Amesema hayo leo katika hospitali ya taifa Muhimbili (MNH), alipokua katika maadhimisho ya mtoto njiti duniani ambayo huadhimishwa  novemba17 kila mwaka.
Pia mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya taifa Muhimbili(HNM)profesa Lawrence Museru amesema kua hospitali hiyo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali inaendelea kutoa mafunzo ya mda mfupi na mrefu kwa wauguzi na madaktari wa kitengo cha watoto wachanga ili kuongeza ufanisi wa kazi.

No comments

Powered by Blogger.