Heade

MUUNGANO WA UPINZANI NCHINI CONGO WAITISHA MAANDAMANO

Muungano wa Upinzani wa Rassemblement nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo umeitisha maandamano ya nchi nzima hivi leo kumshinikiza rais Jospeh Kabila kuondoka madarakani kufikia mwisho wa mwaka huu.

Upinzani pia unataka kuwepo kwa serikali ya mpito kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka ujao.

Mwenyekiti wa muungano huo Felix Tshisekedi pia ametupilia mbali mswada wa sheria za uchaguzi na kusema kuwa zinahatarisha mchakato mzima na wakati huo huo kuwataka wananchi wajitokeze kwa uwingi kuhishiriki maandamano ya hii leo.

Hata hivyo serikali ya DRC imepiga marufuku maandamano hayo ikisema kuwa ni kutokana na sababu za kiusalama.

Kumekuwa na shinikizo kutoka kwa Jumuiya ya Kimataifa, kwa serikali ya DRC kuhakikisha kuwa Uchaguzi huo unafanyika kama ilivyopangwa.

Polisi jijini Kinshasa katika siku zilizopita, wamekuwa wakikabiliana na waandamanaji wa upinzani kwa kuwakamata na hata kuwafwatulia risasi na mabomu ya kutoa machozi.

Watu kadhaa walikamatwa na wengine kujeruhiwa katika mandamano yaliyofanyika hivi karibuni katika miji ya Goma na Bukavu, mashariki mwa DRC, kumshinikiza rais Kabila ajiuzulu kabla ya tarehe 30 Desemba mwaka huu.

No comments

Powered by Blogger.