Heade

MWANA CHUO MMOJA AJINYONGA TABORA




 Mwanachuo mmoja wa chuo cha utumishi wa umma tawi la Tabora anayefahamika kwa jina la Raphael Kadesha (22) amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia tai ya kuvaa shingoni.
Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora  Graifton Mushi amesema tukio hilo limetokea jana asubuhi ambapo marehemu alifunga tai juu ya kitanda chake.
Amesema marehemu alikua mwanafunzi wa kozi ya Utawala ngazi ya cheti katika chuo hicho na kusema chanzo cha kifo chake bado  hakijajulikana na jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi.
Naye mkurugenzi wa chuo hicho Dk Ramadhani Marijani amewataka wanachuo kuwa watulivu wakati jeshi la polisi kuendelea na uchunguzi.

No comments

Powered by Blogger.