Heade

RAIS WA KENYA UHURU KENYATA ATARAJIWA KUAPISHWA



Rais wa kenya mhe, Uhuru Kenyatta anatarajiwa kuapishwa kuwa rais kwa muhura wa pili baada ya mahakama ya juu kufutilia mbali kesi ambazo zilikuwa zinapinga ushindi wake katika uchaguzi wa marudio uliofanyika tarehe 26 october mwaka huu.
Aidha kifungu cha 141 (1b) cha katiba ya kenya kinasema rais anafaa kuapishwa siku ya saba inayofuata  siku ya kutolewa kwa uamuzi wa mahakama wa kuidhinisha uchaguzi iwapo kukiwa na kesi iliyokuwa imewasilishwa.
Hata hivyo kwa mujibu wa katiba rais anafaa kuapishwa hadharani mbele ya jaji mkuu au naibu jaji mkuu.

No comments

Powered by Blogger.