Heade

USAID YAIPONGEZA SERIKALI YA TANZANIA KWA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI



Mkurugenzi mkazi wa shirika la misaada ya kimataifa la marekani USAID bwana Andy Karas amepongeza jitihada za serikali ya tanzania kupitia mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF katika kuwafikia wananchi wanaokabiliwa na umaskini kupitia mpango wa kunusuru kaya maskini ambao umeanza kuonyesha mafanikio makubwa katika maeneo mbalimbali nchini.
Bwana Karas ameyasema hayo wakati alipokutana na walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini katika kijiji cha Igingilanyi kata ya Nduli katika halimashauri ya wilaya ya Iringa ambako licha ya kuelezwa namna TASAF inavyoendelea kutekeleza mpango huo lakini pia ameshuhudia namna walengwa wa mfuko huo walivyoboresha maisha yao kwa kutumia fedha za ruzuku za mfuko huo.
Amesema kuwa hamasa inayoonyeshwa na walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini katika kujiletea maendeleo kwa kuanzisha miradi midogomidogo kwa kutumia fedha zinzotolewa na serikilali kupitia tasaf imelivutia shirika hilo na kuahidi kuwa litaendelea kushirikiana na serikali ya tanzania katika kuboresha utaratibu wa kuwainua wananchi kiuchumi.
Hata hivyo bwana karas amesema utaratibu wa kuwafikia na kuwasaidia moja kwa moja wananchi wanaoishi katika mazingira magumu ya kiuchumi umekuwa ukitumika katika nchi nyingi duniani na umeonyesha mafanikio makubwa kwa kusimamia shughuli za kiuchumi na kijamii kwa kaya maskini.


No comments

Powered by Blogger.