Heade

ALIYEKUWA MAKAMU WA RAIS NCHINI ZIMBABWE ANATARAJIWA KUAPISHWA KUWA RAIS WA NCHI HIYO



 Aliyekuwa Makamu wa Rais nchini Zimbabwe Emmerson Mnangagwa anatarajiwa kuapishwa kuwa rais wa nchi hiyo baada ya Rais Mugabe kujiuzulu.

Rais Robart Mugabe amejiuzulu kishingo upande baada  ya kuwepo kwa mvutano ulioibua mgogoro wa kisiasa nchini humo na kupelekea jeshi kuchukua udhibiti wa mamlaka .
Spika wa bunge nchini Zimbabwe amesema hatua hiyo ni ya kujitolea na amefanya hivyo ili kuweza kuwepo kwa mabadiliko mazuri ya mamlaka.
Wabunge wamefurahia hatua hiyo baada ya kupokea taarifa ya spika wa bunge na raia wamejitokeza barabarani  kusheherekea.

No comments

Powered by Blogger.