Heade

WANANCHI WA WILAYA YA TARIME WATAKIWA KUTUMIA MPAKA WA SIRARI VIZURI



Naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mhe. Hamadi Masauni amewataka wananchi na wafanya biashara wanao fanya shughuri zao karibu na kituo cha mpaka  wa sirari unao tenganisha  nchi ya Tanzania na kenya kuhakikisha wanashirikiana na jeshi la polisi mkoani mara kudhibiti matukio ya uhalifu.
Ameyasema hayo akiongea na wananchi wakati wa ziara yake ya kikazi katika mkoa wa mara ikiwa na lengo la kutembelea mipaka iliyopo mkoani mara inayo tenganisha Tanzania na nchi jirani za kenya na uganda ambapo amesema kuwa mara nyingi kumekuwa na taarifa za wananchi wa mipakani kushirikiana na uhalifu kupitisha mali za magendo suala ambalo ni hatari.
Hivyo amewataka wananchi hao kuwacha tabia hiyo inayokuwa kwa kasi katika eneo la mpaka na kulisisitiza jeshi la polisi kufanya kazi yake kikamilifu na kwa yeyote atakae baina kutumia mpaka kinyume na utaratibu atakumbana na mkono wa sheria.

No comments

Powered by Blogger.