Heade

VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WASHIRIKISHWA KATIKA MAAMUZI




MWENYEKITI wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Semistocles Kaijage amewataka wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi nchini kuwashirikisha viongozi wa vyama vya siasa katika maamuzi yenye maslahi ya pande zote ili kuendeleza amani na utulivu nchini.
Akizungumza na wasimamizi wa uchaguzi Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Jaji Kaijage amesema katika kipindi hiki ambacho vyama vinashiriki kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Udiwani Jumapili hii, ni muhimu wasimamizi wa uchaguzi kuhakikisha maadili ya uchaguzi wakati wa kampeni yanazingatiwa ili kuepusha uvunjifu wa amani miongoni mwa wananchi.
Jaji Kaijage ambaye yuko katika ziara ya kutembelea mikoa ya Tanga, Kilimanjaro na Arusha kushuhudia utekelezaji wa Maadili ya Uchaguzi katika Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Udiwani, aliwataka wasimamizi wa uchaguzi kuhakikisha vifaa vyote ambavyo vinahitajika ili uchaguzi ufanyike vimepatikana na vile ambavyo havijapatikana wawasiliane na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kasoro zinazobainika zipatiwe ufumbuzi kabla ya siku ya uchaguzi.

No comments

Powered by Blogger.