Heade

WAZIRI MKUU WA LEBANON AYAPA UHAKIKA MABENKI




Waziri Mkuu wa Lebanon Saad Hariri amewahakikishia wadau wa mabenki katika eneo la Mashariki ya Kati hii leo kuwa suala la uthabiti wa Lebanon ndilo lenye umuhimu mkubwa kwa upande wake. Matamshi hayo ya Hariri yanakuja ikiwa ni siku moja tangu arejee nchini humo na kusitisha tangazo lake la kujiuzulu alilolitoa wakati akiwa nchini Saudi Arabia na kusababisha mkwamo wa kisiasa nchini humo.
 Akizungumza katika kongamano la mabenki la nchi za Kiarabu mjini Beirut, Hariri amesema serikali yake itatoa kipaumbele kwa masuala yenye masilahi na nchi hiyo zaidi kulinganisha na changamoto zinazokabili ukanda huo.
Aidha  Kundi la wabunge wa chama cha Hezbollah nchini Lebanon katika taarifa yake limesema hii leo kuwa kurejea kwa Saad Hariri na kauli yake ya matumaini kunaashiria hali kurejea kuwa ya kawaida nchini humo.

No comments

Powered by Blogger.