Heade

WAZIRI WA MALI ASILI NA UTALII ATOA AGIZO



Katibu mkuu wa wizara ya mali asili na utalii mh. Gaudence Milanzi amesema agizo la waziri wa mali asili na utalii Mh Hamis Kigwangalla  kuhusu kusimamishwa kazi mkurugenzi wa wanyama poli profesa Alexander Songorwa  litatekelezwa baada ya utaratibu kufuatwa.
 Dk Kigwangallah aliagiza profesa Songorwa  kusimamishwa kazi kutokana na tuhuma kadhaa  baada ya kufanya ziara katika hifadhi ya taifa ya serengeti ambapo aliieleza taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa Takukuru kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo na hatua sitahiki zichukuliwe.
Hata hivyo mwaka 2014 mkurugenzi huyo alisimamishwa kazi na aliyekuwa waziri wa wizara hiyo Lazaro Nyalandu kutokana na kutajwa katika operesheni tokomeza na kamati ya bunge ya ardhi, maliasili na utalii ambapo baadae alirejeshwa kazini.

No comments

Powered by Blogger.