JESHI la Polisi mkoani Pwani limesema kuwa baadhi ya wanafunzi wa
shule za sekondari na msingi, walioripotiwa kupotea mkoani humo hususani
katika eneo la Kibiti, wameanza kupatikana.
Mwishoni mwa mwezi uliopita, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP),
Simon Sirro alifanya ziara ya kikazi mkoani Pwani na kuagiza kufanyiwa
kazi kwa madai ya kupotea kwa karibu watoto 1,300 mkoani humo ili
ijulikane wamekwenda wapi.
Gazeti hili lilipotaka kujua ni kwa kiasi gani agizo la IGP
limefanyiwa kazi, Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Jonathan Shana alisema
kuwa baadhi ya watoto hao wamepatikana. Alisema waliopatikana ni wale
waliokuwa watoro shuleni.
Bila kutaja idadi yao, Kamanda Shana alisema wanafunzi hao
wamerudishwa kwa wazazi wao na wanaendelea na masomo. “Tunaendelea
kuwatafuta wanafunzi wengine waliobaki kwa kushirikiana na maofisa elimu
wa wilaya na kata. Tuliowapata walikuwa ni watoro tu shuleni na
tumeshawakabidhi kwenye shule zao wanaendelea na masomo,”alieleza
Kamanda Shana.
Mbali na hao waliopatikana, Kamanda Shana alisema kuwa Polisi
inaendelea kufuatilia zaidi taarifa za baadhi ya watoto 1,300 waliopotea
Kibiti waanza kurejea hao, kupelekwa nje ya nchi kwa mafunzo
yanayodhaniwa kuwa ya kutumia silaha. Alisema mara nyingine watoto
hupelekwa nje ya nchi kwa kigezo cha kupewa mafunzo ya dini, lakini
baadae hubainika kujifunza mambo tofauti ikiwemo matumizi ya silaha.
No comments