Heade

MAMBOSASA ATAKA ASKARI KUFANYA MAZOEZI

KAMANDA wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amewataka askari kufanya mazoezi ya viungo ili kujiweka imara sambamba na kujenga afya zao.

Kamanda Mambosasa aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam, wakati aliposhiriki katika matembezi na mazoezi ya viungo na askari wa vikosi vya Kanda Maalumu ya Dar es Salaam. Alisema askari na jamii kwa ujumla wanapaswa kufanya mazoezi pale wanapopata nafasi na siyo mpaka walazimishwe, kwani mazoezi yanasaidia kujenga mwili na kuepusha mwili na magonjwa yasiyoambukiza kama kisukari na shinikizo la damu.

“Mazoezi haya yanatakiwa kuwa endelevu kwa askari wote wa polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, mazoezi haya yanajenga urafiki na kuimarisha ujirani mwema na pia yanaweka mwili imara,” alisema. Matembezi hayo ya ‘Root Match’ yalifanyika katika mikoa ya kipolisi Temeke na Kinondoni na yatakuwa yakifanyika kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi











































No comments

Powered by Blogger.