Heade

ONYO ZAENDELEA KUTOLEWA KABLA YA MAAMUZI YA RAIS DONALD TRUMP KUHUSU JERUSALEM


Rais wa Marekani Dnald trump anaendelea kukabiliwa na vitisho vya kuvunjika kwa uhusiano wa kidiplomasia wa nchi hiyo na jumuiya ya nchi za Kiarabu kufuatia nia yake ya kutaka kuhamishia ubalozi wa Marekani nchini Israel katika mji wa Jerusalem kutoka mji wa Tel Aviv.

Kama kweli atachukua uamuzi huo kama alivyomtaarifu kiongozi wa Mamlaka ya Palestina Mahmoud Abbas na Mfalme wa Jordan au kuutambua mji huo mtakatifu kama mji mkuu wa Israel, Donald Trump atakua amekwenda kinyume na msimamo wa jumuiya ya kimataifa na viongozi wengi waliomtangulia katika uongozi wa taifa la Marekani. Nchi za Kiarabu zimeendelea kutoa onyo kufuatia hatua hiyo ya Marekani.

Ikulu ya White House imethibitisha kuwa rais Donald Trump atazungumza leo Jumatano kuhusu uwezekano wa kuhamishia ubalozi wa Marekani Jerusalem.

Kwa mujibu wa msemaji wa ikulu ya white house Sarah Sanders amesema kuwa Trump alizungumza na baadhi ya viongozi siku ya jumanne kuhusu mpango wake ya kuhamishia ubalozi huo kutoka tel aviv kuupeka Jerusalem.

Viongozi wa Palestina, Misri, Jordan na saudi arabia, wametoa onyo kwa rais Trump kuwa kuhamishia ubalozi huo Jerusalem kutadhoofisha kabisa juhudi za kuleta amani Mashariki ya Kati.

Siku ya Jumanne rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alisema kuwa ana wasiwasi kuwa rais huyo wa Marekani anaweza kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

Israel na Palestina wote wanadai kuwa mji huo ni mji wao mkuu.

Israeli ilivamia eneo hilo la Mashariki mwa Palestina mwaka 1967 na kulifanya kama eneo lake baadae. Uamuzi huu hautambuliwi kimataifa. Israeli inaona mji huo kuwa mji wake mkuu.

Kwa upande wao, Wapalestina wanadai Jerusalem ya Mashariki kama mji wao mkuu wa baadae.

No comments

Powered by Blogger.