SERIKALI kupitia Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangala
imeunda kamati maalum ya watu waliobobea katika mambo ya ubunifu wa
mikakati ya masoko, mawasiliano, mahusiano kwa umma, utalii na biashara.
Kigwangala katika taarifa yake aliyoituma kwa vyombo vya
habari na mitandao ya kijamii, amesema lengo kuu la kamati hiyo ni
kuanzisha mchakato wa kitaalam (technical) wa kuandaa utambulisho mpya
wa Tanzania kwenye masoko ya kimataifa ya Utalii.
Amesema kuwa Kamati hiyo inakusudiwa kufanya uchambuzi wa kina wa
tafiti mbalimbali na kukusanya maoni kutoka kwa wadau muhimu kisha
kuzipeleka kwake mapendekezo yao.
“Kamati hii inakusudiwa kufanya uchambuzi wa kina wa tafiti
mbalimbali na kukusanya maoni kwa wadau mbalimbali muhimu kisha
kuniletea mapendekezo yao,”alisema Kigwangala.
Aidha amesema kuwa licha ya kuwa Malisili na Utalii sio Wizara ya
Muungano lakini masula ya Utalii kwa pande mbili za Tanzania Bara na
Zanzibar ni vitu ambavyo katika utekelezaji haviwezi kukwepana na
huchangia kudumisha muungano huo, hivyo Kamati inahusisha pia wajumbe
kutoka Zanzibar.
“Maliasili na Utalii siyo Wizara ya Muungano na kwamba utalii,
kimsingi ni katika mambo yatakayodumisha zaidi Muungano wetu na Umoja
wetu, sababu kimkakati na kiutekelezaji hatuwezi kukwepana, na kwamba
uuuzaji wa vivutio vya utalii ni katika mambo ya kufanywa kwa pamoja ili
kuwa na tija kwa Taifa letu,” amesema Kigwangala.
Amesema kuwa alipokea ushauri kwamba ni vema toka hatua za awali
kamati hiyo kuweka wajumbe wa kutoka serikali ya Mapinduzi Zanzibar
kwenye Kamati hiyo.
“Awali tulikuwa na fikra kwamba baada ya kazi za mwanzo kufanyika na
kuwa na andiko la kitaalamu la kufanyia kazi, tungeanzisha mawasiliano
rasmi ndani ya Serikali zetu mbili, ambapo kungekuwa na majadiliano
ngazi ya wataalam na baada ya hapo ngazi ya Mawaziri,” amesema
Kigwangala na kuongeza kuwa bado wa nampango wa kufanya hivyo.
Utamaduni uliojengeka wa kufanya kzi kwa pamoja kwa ukaribu kwenye
kutangaza vivutio vilivyopo sehemu zote mbili za Muungano utaendelea
kufanyika hivyo kwani watalii wanaokuja kwenye mbuga hupenda kwenda
Zanzibar kufanya utalii wa fukwe na wa kiutamaduni, na wale wanaofika
Zanzibar nao hutaka kuja Tanzania bara kutembelea vivutio vingine vya
utalii.
Amesema yeye binafsi ni muumini mkubwa na mahiri wa Muungano, na
utangamano kwa ujumla wake na ushirikishwaji kama zana muhimu ya
kufanyia maamuzi nyeti, hivyo hawezi kuwa wa kwanza kukiuka msingi wa
imani yake kama kiongozi.
Hivyo amesema pindi hatua stahiki zitakapofikiwa atakaa na Waziri
mwenzake wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kushauriana na kukubaliana.
No comments