KUU wa wilaya ya Tanga, Thobias Milapwa amewaahidi wafanyabiashara wa
gulio la Tangamano kwamba amepokea na atafikisha kwenye mamlaka husika
ombi lao linaloitaka halmashauri ya jiji kupunguza ushuru kutoka sh.
1,500 mpaka 500, kurasimisha na kuboresha mazingira ya eneo hilo ili
wawezekuchangia ipasavyo maendeleo ya nchi.
Alikuwa akizungumza na wafanyabiashara hao ili kuzindua mradi wa
kuendesha semina za kutoa elimu kwa mlipakodi mkoani Tanga inayolenga
kuwatambua na kuwasajili wafanyabiashara walio katika sekta isiyo rasmi
inayoratibiwa na mamlaka ya mapato (TRA).
"Ninachoweza kusema kuhusu ombi lenu hilo nimelipokea lakini uamuzi
wake sinao hapa kwasababu niwa kisera hivyo lazima lipitie mchakato wa
maamuzi ya watu wanaotajwa kisheria vikiwemo vikao vya baraza la
madiwani wa Halmashauri ya jiji la Tanga", alisema.
No comments