Heade

UMOJA WA ULAYA WATISHIA KUSITISHA MISAADA YAKE DRC

Umoja wa Ulaya umeionya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya congo kuwa utasitisha misaada yake kusaidia nchi hiyo kufanikisha Uchaguzi Mkuu mwaka ujao, iwapo itaendelea kutumia maafisa wa usalama kuwanyanyansa wanasiasa wa upinzani na mashirika ya kiraia.

Katika ripoti yake Umoja wa Ulaya umesema serikali ya Kinshasa imeendelea kuwakamata, kuwazuia wanasiasa wa upinzani na wafuasi wao pamoja na wanaharakati wa haki za binadamu kwa sababu ya harakati zao za kuikosoa serikali ya rais Joseph Kabila.

Upinzani umefurahishwa na ripoti hiyo. Akihojiwa na RFI, Gregoire Kiro, mbunge wa chama cha upinzani cha RCD-Kml akiwa Kinshasa amesma hatua hiyo itapelekea visa vya unyanyasaji vinavyoendelea kusitishwa mara moja.

Upande wa serikali, wao wanaona kuwa Umoja wa Ulaya hauna sababu ya kutoa mashinikizo yoyote wakati mchakato wa uchaguzi unaendelea vizuri.

Mbali na Umoja wa Ulaya, Ubelgiji ambao ni wakoloni wa zamani wa DRC, wamesema wametenga Euro milioni 5.8 kuisaidia Tume ya Uchaguzi kufanyika hilo.

Tume ya Uchaguzi nchini DRC CENI tayari imetangaza kuwa Uchaguzi Mkuu utafanyika mwezi Desemba mwaka ujao.

No comments

Powered by Blogger.