Umoja
wa Mataifa umesema watoto wapatao 400,000 wapo hatarini kufariki dunia
ndani ya miezi michache ijayo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
DRC kutokana na Utapiamlo.
Hadi
sasa, Utapiamlo nchini humo umewaathiri watoto laki saba na nusu wenye
umri chini ya miaka mitano wengi wao wakiwa hatarini kufariki dunia
mapema mwakani endapo hali ya dharura haitachukuliwa kuwanusuru.
Kaimu
Mwakilishi wa Shirika la kuhudumia watoto (Unicef) Tajudeen Oyewale,
amesema hali hiyo imechangiwa na machafuko ya takribani miezi 18 hali
ilyowalazimu watu kutawanyika na kusababisha uzalishaji wa chakula
kudorora kutokana na watu kuacha kuzalisha chakula ambapo jimbo la kasai
limeathirika kwa kiwango kikubwa.
Aidha, ameongeza kuwa watoto
hao wanakabiliwa na magonjwa yanayosababishwa na utapiamlo na ni vigumu
kufikiwa na huduma za matibabu na lishe inayofaa ili kuokoa maisha yao.
Kwa
mujibu wa Umoja wa Mataifa machafuko kati ya makundi mbalimbali
yanayoipinga serikali nchini DRC yamesababisha maelfu ya watu kupoteza
maisha huku wengine milioni 1.4 wameyahama makazi yao kwa lazima
kutokana na hali hiyo.
No comments